Nimeamua Kwa Hekima

 


 

Mwanakwetu Nimesimama, Nafikiri kwa Makini

Mbungi na Mganda Pia, Zanivutia Moyoni

Kila Moja Ina Sifa, Zenye Mvuto wa Ndani

Najiuliza kwa haraka, Nichague Ipi Mapema?

 

Mbungi Ngoma ya Shangwe, Midundo Yake ya Nguvu

Huwavutia Wengi Sana, Kwa Suati na Miendo

Ni ya Furaha na Vigelegele, Hupamba Sherehe Nyingi

Huenda Nikichagua Hii, Nitawafurahisha Wengi

 

Mganda Nayo Tulivu, Lakini ina Maana

Hufundisha Mila Njema, Na Historia ya Kwetu

Si ya Makelele Sana, Bali Hubeba Busara

Huifanya Jamii Yote, Ijuvunie Asili

 

Moyoni Nafanya Shauri, Nichague Ipi Kwa Haki

Furaha ya Mbungi Kubwa, Lakini Yapaa Haraka

Mganda Ina Uzito, Wa Mila na Heshima

Naona Njia Iliyo Bora, Si Ya Pupa Wala Tamaa.

 

Basi Jibu Nimepata, Bila Kusita Wala Woga

Mganda Ndio Chaguo, Kwa Faida na Kudumu

Nitaianza Mapema, Kwa Bidii na Maarifa

Mwanakwetu Nashukuru, Nimeamua Kwa Hekima

 

Utenzi huu umetungwa na Adeladius Makwega wa Mbagala Mei 10, 2026.

makwadeladius@gmail.com

0717649257

 

 

 

0/Post a Comment/Comments