Adeladius Makwega-MWANZA
Kwa muda mrefu Mwanakwetu amekuwa akikutana na watu wengi wenye
asili ya makabila ya mkoa wa Ruvuma wakiwama Wamatengo, Wakisi, Wamanda ,
Wandendeule na Wangoni, jambo moja zuri alilokutana
nalo ni majina ya ndugu hawa kuwa yanavutia sana kuyasikia, ambayo yanalingana
na majina ya wanyama, ndege na viumbe hai kadhaa.
Kwa hakika viumbe hao wanaopatikana katika mazingira ya
binadamu jirani nao ndiyo majina yao yalichukuliwa na kuwabatiza binadamu kama
yalivyo na mengine kuwekewa viambishi mwanzo aua mwisho .
“Komba, Makomba, Nyakomba, Nyoni, Katembo, Matembo, Nguruwe,
Mkima,Kima, Sungura, Kunguru , Nyoka, Mapunda, Ngonyani, Mbawala, Kiboko na kadhalika.”
Majina haya yamekuwa yakitumika mno si kwa makabaila hayo tu
bali makabila mengi ya kibantu. Mathalani jina SUNGURA linapatikana hata kwa
makabila kama Wafipa .Ndiyo kusema yupo SUNGURA Mfipa na SUNGURA Mngoni na si
adimu kumkuta SUNGURA wa makabila mengine ya pande zote nne za Tanzania.
Majina haya yapo ya aina mbili yale yanayotumiwa majina ya wanyama
hao kwa KISWAHILI mathalani MBAWALA na yapo majina mengine yanayotumia majina ya
asili ya makabila hayo .
Jina la mfano hapa linalotajwa ni NDUNGURU, yapo madai kuwa jina
hilo linamaanisha SIMBILISI ambaye ni mnyama mfupi mdogo anayeishi katika
mashino ardhini.
Mwanakwetu siku ya leo anasema nini?
Mwanakwetu anakuomba msomaji wake utambue mambo yafuatayo katika
majina hayo.
Kwanza wanyama hao walikuwa wakipatikana katika mazingira
jirani na huyo binadamu anayeitwa jina la Mnyama huyo.
Majina hayo yalitolewa kwa sababu ya baadhi ya tabia za
binadamu zinazolingana na wanyama hao.
“Mathalani Tembo, Matembo, Katembo–Tabia za Nguvu za TEMBO.”
Hoja nyingine inayotolewa hapa ni baadhi ya watu kupachikwa majina
hayo ilitokana na watu hao kujificha ugeni wao na kuonekana wao pia ni wenyeji
wa eneo hilo.
Ndiyo kusema hata akina KOMBA na MAPUNDA walikuwa na majina ya
koo zao mengine na majina yalivuma na kuenea ni haya ya wanyama.
Kuficha huko asili yao kulisadia wao kuonekana wenyeji na kuwa salama wao na familia
zao.
Mwanakwetu Upo?
Hiyo ndiyo sababu ya binadamu kuitwa majina ya wanyama.
Nakutakia siku Njema
0717649257
Post a Comment