Adeladius Makwega-MWANZA
Mwanakwetu kwa juma zima umeme umekuwa shida kubwa hapo Malya,
hivyo kidogo imekuwa ngumu simu yake ya mkononi kuhifadhi umeme, hata kusoma
baadhi ya taarifa imekuwa vigumu.
Jumamosi ilipita umeme ukiwa wa mashaka mashaka na ulikatika tena
na ulirudi jumapili ya Septemba 3, 2023 Jioni.
Uliporudi umeme jumapili hii alifanya shughuli zake haraka
haraka alafu akasema ngoja niingie katika mtandao ya kijamii na huko alikaribishwa
na ujumbe huu,
“Nilikufahamu mwaka 1992. Tukafunga ndoa 1994.
Tumeishi miaka 29 tu Mwenyezi Mungu amekutoa kwangu. Upumzike kwa Amani Mume
wangu, mshauri wangu na rafiki yangu. Tutaonana baadaye.”
Ujumbe huo ulipachikwa katika ukurasa wa mtandoo
wa kijamii wa Mtangazaji na Mtayarishaji Vipindi wa TBC, ndiye Mkuu wa wa Idhaa
ya TBC Taifa kwa sasa Shida Masamba ambaye awali alikuwa akifahamika kama Shida
Waziri, huku jina lake lilibadilika kuwa Shida Masamba baada ya kuolewa na
Profesa Masamba nguli wa Kiswahili nchini Tanzania na ambaye ameshiriki
kutayarisha kamusi nyingi za lugha hii.
Hapo Mwanakwetu alibaini kuwa kumbe Profesa
Masamba Masamba amefariki dunia.
Mwanakwetu alimtumia ujumbe wa Pole Mtangazaji &
Mtayarishaji Vipindi wa TBC Shida Masamba.
Taarifa hiyo ya msiba ilimbeba mzega mzega
Mwanakwetu hadi katika mambo kadhaa ya miaka mingi nyuma.
Mosi,
“Mwaka 2003 Mwanakwetu alikuwa akifundisha somo la Kiswahili katika
shule moja binafsi ya Kimataifa iliyokuwa na Shule ya Msingi na Sekondari
kuanzia darasa la Saba na Kidato cha Kwanza hadi ya Nne. Huku Mwalimu Mwenzake
mmoja kike akisomesha somo hilo Darasa la tatu hadi la sita. Profesa Masamba
wakati huo alikuwa na Kijana wake wa kiume mwenye jina lake (Masamba Masamba), mwaka
2003 alikuwa darasa la tatu, Mwalimu mwezake Mwanakwetu aligafilika na
kuweka mkasi badala ya vema katika swali
mojawapo la somo la Kiswahili. Hilo lilimtoa Profesa Masamba Chuo KIkuu cha Dar
es Salaam na alifika shuleni hapo na kuidai alama ya kijana wake mdogo. Huku
jambo hulo liliongeza umakini mkubwa kwa walimu wa shule hii akiwamo Mwanakwetu
ambaye wakati huo alikuwa ndiyo amehitimu Stashahada wa Ualimu kutoka Chuo cha
Ualimu Kasulu Kigoma sasa ni zaidi ya miaka ishirini iliyopita.”
Mzega mzega huo wa simanzi ulimbeba Mwanakwetu
hadi akakumbuka kuwa alipokuwa mtumishi wa Shirika la Utangazaji Tanzania alikuwa
akifanya kazi kwa karibu sana na Shida Masamba ambaye wakati huo alikuwa ndiye
mpangaji vipindi vinayokwenda hewani na akiwa na jukumu la kuvisikiliza kabla
ya kwenda hewani, pia alikuwa Mtayarishaji wa Kipindi cha Husia wa Baba.
“Kama siyo Juhudi zako Nyerere, kama Siyo Juhudi Zako
Nyerere, Mshikamo tungetoa wapi.”
Msomaji wangu huyu huyu Shida Masamba ndiye
aliyeundika ujumbe huo na mke wa Profesa Masamba ambaye leo hii amefiwa na
mumewe. Mwanakwetu akakumbuka hata Wazazi wa Shida Masamba akiwamo Mzee Waziri
mwenyewe walikuwa wakikaa Mbagala ambapo Mwanakwetu alishafika mara kadhaa.
(Shida Masamba)
Mwanakwetu alikumbuka hata baadhi ya vipindi
alivyowahi kutayarisha na Bi Shida Masamba zikiwamo hata jingles za Mwalimu
Nyerere ambazo hadi kesho zinachezwa na TBC Taifa, Ikiwamo ya Mgiriki aliyetiwa
ndani ya Mwalimu Nyerere.
Mzegamzega huo wa simanzi uliendelea kumteka
Mwanakwetu akakumbuka,
“Wakati wa Ramadhani ya kila mwaka, Shida Masamba alikuwa na
utaratibu wa kila kumi la mwisho kuwaalikia baadhi ya wafanyakazi wenzake na majirani
kwenea kufuturu nyumbani kwake Mwenge Dar es Salaam. Mwanakwetu japokuwa Mkristo
kila mwaka alialikwa na hiyo fursa kila mwaka aliitendea haki ipasavyo. Huko
Mwanakwetu alikutana na Profesa Masamba na mwanafunzi wake Masamba Masamba yule
aliyepokwa alama akiwa darasa la tatu na wakati huo alikuwa Chuo Kikuu huko
Uchina.”
Mwanakwetu akiwa na mzegamzega huo simanzi
anasema nini?
Kwa heshima zote anatoa pole kwanza kwa Shida
Masamba kwa kufiwa na mumewe, anatoa pole kwa mwanafunzi wake Masamba Masamba
kwa kumpoteza baba yake mzazi ambaye alijali mno elimu ya mtoto wake japokuwa alikuwa
Profesa wa Chuo Kikuu akiwa na majukumu mengi, Mwanakwetu pia anatoa pole kwa
familia nzima ya msomi huyu popote ilipo kwa kumpoteza ndugu yao
Buriani Profesa Masamba.
0717649257



Post a Comment