Adeladius Makwega-MWANZA
Chama cha Mapinduzi
kinapofanya mikutano yake ya ngazi za chini na ile ya kitaifa kimekuwa na taswira
mbili fofauti zinayojengeka machoni mwa yule anayefuatilia mikutano hiyo.
“Unapoutazama mkutano wa kitaifa
unakutana na picha za wajumbe wote wakiwa wamependeza sana na sare zao zinawakawaka
na wakisindikizwa na bashasha katika mapaji ya nyuso zao.”
Wajumbe hao wakizungumza kwa
furaha na ni mara chache mno kuona mjumbe wa CCM katika mikutano hiyo ya kitaifa akipinga jambo hadharani, utamaduni
huo huwa ni ni mwiko kwa vikao hivyo kusikia msamiati hapana mara nyingi mambo
huwa ni ndiyo.
Swali la kujiuliza Je taswira
ya mikutano ya kitaifa ya CCM ndiyo taswira ya mikutano ya CCM ngazi za chini?
“Taswira ya wajumbe katika
vikao vya chini huwa ni wale waliovalia sare zilizochaka, kupauka na kuchujuka
mno, huku wengine wakijaliwa kuwa na labda kofia ya CCM tu, mwingine akijaliwa kuwa
na shati tu rangi ya kijani au njano huku sketi au suruali ikiwa ya rangi
nyengine.”
Hizo
ni sura mbili tofauti lakini chama cha siasa kile kile chenye bendera moja
yenye kijani tupu lakini ina nendo yake za nyundo na jembe.
“Loooo salaleeee! hiki ni chama cha
Mwanakwetu.”
Panapomalizika vikao hivyo vya
chini hoja ya kuwarejesha wajumbe mashinani kwao ikiwa ngondo, wengine wakirudi
majumbani mwao kwa miguu, pengine kukosekana kwa mtu wa kutoa hisani ya wajumbe
hao kurudi majumbani kwa kutoa basi au lori. Huku jambo la msingi la wao
kukamilisha akidi ya kikao likiwalimefanyika. Wajumbe na viongozi wa CCM
kutokana ngazi za chini hata wao wanapoitazama taswira ya mikutano ya kitaifa
ya chama chao inawavutia mno na wao kutamani kuwa miongoni mwa wajumbe hao,
Mwanakwetu hiyo kwao huwa ni
fahari ya macho tu wanaona katika kideo tu, kuomba kura na kufika huko ni kazi
nzito mpaka kuwaona wajumbe wote na kuwapatia maboresho ni zoezi zito ambalo
Mwanakwetu haliwezi, zoezi hilo linaitaji mtu awe mfuko uliojaa mapesa.
“Mwanakwetu fukara wa kutupwa,
hapo lazima uwe Lodi.”
Mwanakwetu akiwa katika
tafakari nzito juu ya chama hiki kilichozaliwa na TANU na ASP vyama viliyowakombea
wanyonge anafananisha taswira hiyo ya chama hiki na EMBE DODO UPANDE.
Msomaji wangu pengine wewe ni
mgeni wa Embe Dodo Upande !
“Kuna
aina mbili za embe dodo; Dodo ya Kawaida ambayo huwa embe kubwa chachu kidogo
ikiwa mbichi na ikiiva ni tamu sana, pande zote hadi kokwa. Aina ya pili ni ya
Embe Dodo ni Embe Dodo Upande hii
huwa inafanana na Dodo ya Kawaida bali chachu sana ikiwa mbichi na hata ikiiva
huwa na uchachu na utamu kidogo.Ukifika maeneo ya pwani kama vile Mkuranga,
Mkamba, Kiziko, Kisere, Magoza, Kiparang’anda na mwanadilatu Dodo Upande
inatumika sana kutengeza siki na chachandu ambayo kidogo inakuwa kiungo cha kuongeza hamu ya kulia chakula tu.
Hiyo ndiyo kazi kubwa ya Embe Dodo Upande kutengeneza siki na chcahandu ya
kulia chakula, thamani yake siyo sawa na Embe Dodo la Kawaida.”
Mwanakwetu Upo?
Ndiyo maana Wazaramo, Wakwere,
Wandengereko, Wamakonde, Wapogoro na Warugulu hii Embe Dodo Upande hiyo
ndiyo kazi yake.
Jukumu la viongozi wa sasa wa
CCM bila ya kutafuna maneno wanayo kazi ya kuubadilisha huu Muembe
Dodo Upande uwe Muembe Dodo wa Kawaida, kazi kwao. Mwanakwetu
kwa mapenzi ya dhati kwao anawapa mbinu moja waubatize huo muembe mara moja ili
matawi yake yasizae Embe Dodo Upande tena.
Nakutakia siku Njema.
0717649257







Post a Comment