WASIOJULIKANA AINA MPYA YA USHIRIKINA

 

 


Adeladius Makwega -MBAGALA

 

“Ninayo furaha kubwa sana kupata fursa ya kuadhimisha Ibada ya Ekaristi katika Kanda hii ya Ziwa. Ninatoa shukrani kwa Askofu Mkuu Anthony Mayala kwa maneno yake mazuri ya kunikaribisha, na ninawasalimu kwa upendo mkuu ndugu zangu Maaskofu, mapadri, watawa na walei wote wa Jimbo Kuu la Mwanza na wa Majimbo ya Bukoba, Geita, Musoma, Rulenge na Shinyanga. Pia ninawasalimu kwa namna ya pekee viongozi wa Serikali na wa siasa, wawakilishi wa Jumuiya mbalimbali za kikristo na wa madhehebu mengine na watu wote.

 

Haya yalikuwa maneno ya  sentensi ya pili iliyozungumzwa kwa Kiswahili na Baba Mtakatifu Yohane Paulo wa II(Mtakatifu Yohane Paulo II) alipokuwa katika Jimbo Kuu Katoliki la Mwanza Septemba 4, 1990. Akiendelea kuongea katika ardhi ya mkoa wa Mwanza hapa hapa Tanzania, katika sehemu ya mwisho ya mahubiri yake aya ya nne Baba Mtakatifu Yohane Paulo II alisema maneno haya,

 

“Kwa kutii amri ya Bwana—‘Mpendane kama nilivyowapenda ninyi’ nyinyi, Wakristo wa Kanda ya Ziwa, mnachangamoto ya kufikiria kuhusu hali katika nchi yenu wenyewe. Je, wazee, wajane, walemavu na wapweke hupata kati yenu uelewa na usaidizi wanaohitaji ? Je, utu wa kibinadamu wa watu wote huheshimiwa sikuzote? Au je inatishwa na mazoea kama vile uchawi au uchawi huwaongoza wale wanaojihusisha nayo kwenye aina za utumwa na ibada za uwongo? Kadhalika pamoja na kwamba kuna maadili mengi ya kweli na yanayosifiwa ya kibinadamu yanayohusiana na mila za ndoa za kimila kama vile mahari, je, kukithiri kwa matumizi mabaya ya mila hizi hayasababishi mitazamo inayohukumu utu na thamani ya mtu kwa misingi ya mali na mali tu? ”

 

Haya yote yanadokezwa na Dkt Simeon Mesaki Raia wa Tanzania wakati akifanya utafiti wake wa Shahada ya Uzamivu (PHD) wenye jina Uchawi na Mauaji ya wachawi Tanzania wa Chuo Kikuu cha Minnesota mwaka 1993.

 


Mwanakwetu anajiuliza tangu Baba Mtakatifu Yohane Paulo wa II afike Tanzania mwaka 1990 hadi leo si miaka mingi? Jibu ni miaka 34 kama ni mingi au michache msomaji wangu jibu unalo.

Swali lengine la Mwanakwetu je vijana waliozaliwa Mwanza/Tanzania baada ya ugeni huo je msimamo huo wa Vatikani kwa Mwanza je wanaufahamu? Je ujumbe wa Vatikani kwa Mwanza umeweza kuibadilisha jamii hii na kuachana na Imani za Kishirikina? Hilo ni swali ambalo lazima liwe na majibu.

Kwa hakika Mwanakwetu yupo mkoani Mwanza sasa kwa karibu mwaka mmoja na miezi sita hoja ya ushirikina bado ipo na tena hata kwa vijana waliozaliwa baada ya ujio wa Baba Mtakatifu Yohane Paulo wa II.

 

“Mtani hao mbuzi na kondoo wako usipotumia dawa za jadi kwa hakika watakufa wote, jitahidi kutuona wenyewji tukupatie dawa za mifugo za kimila ili mifugo yako ibaki salama. Hapa watu wengine wanaiangalia kwa kijicho hakuna mtu anayependa wewe ufuge upate mbuzi na kondoo wengi.”

 

Haya maneno anaambiwa mtayarishaji wa makala haya mapema Januari 2024 imani ya ushirikina bado imekita kambi.Isitoshe hata kitendo cha Padri wa Kanisa Katoliki wa Kanda ya zimwa kukamatwa kwa tuhuma za mauwaji ya binti mwenye ualibino hiyo ni kengele inayoonesha ushirikina umekita kambi katika ardhi ya Tanzania. Mwanakwetu akiishia kuitazama mifano ya Kanda ya ziwa tu hilo halitokuwa haki, ebu tilia maanani kisa hiki,

 

“Nikiwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halimashauri ya Lushoto mwaka wa 2017. Siku moja niliamka asubuhi na kukuta mifugo yangu kadhaa imeuwawawa ikiwamo mbuzi, kuku paka na ngombe. Hili lilikuwa tukio la kushangaza inakuje mifugo hiyo ife kwa wakati mmoja?Je imelishwa sumu. Nikajitahidi , nikavijulisha vyombo vya Ulinzi na Usalamana baadaye kuelekea kazini na nilipofika katika jengo la Halmashauri baad ya kushuka katika gari nikakuta kundi la wafanyakazi wapo mlangoni, wakisita kuingia ofisini , maana wamekuta damu zimemwagwa katika mlango. ‘Mkuu damu zimemwagwa koridoni usivuke ngoja kwanza .’ Mkurugenzi akasema labda mbwa alikuwa anawinda usiku akabeba windo lake akalila katika sakafu za Halmshauri.Wafanyakazi hawaamini hicho kinachosemwa na mkurugenzi.’ Wafanyakazi wanajibu hapana huu ni ushirikina.Mkurugenzi kasahau kwake mifugo yake imeuwawawa. Usafi ukafanyika huku mkurugenzi Mtendaji akiingia kupitia mlango wa dharula.

Jambo hilo likaleta taharuki kubwa wengine wakisema wanyama waliuwawawa nyumbani kwa kiongozi damu yake ndiyo iliyomwagwa sakafuni ofisini nia ni kumroga Mkurugenzi Mtendaji, kwa kuwa washirikina hao waliamini mnapotaka kumroga mtu wa PWANI Tanzania basi kumroga ili alorogeke vizuri unamroga kwa wanyama wake mwenyewe.”

 

Mkurugenzi Mtendaji husika aliongezwa Ulinzi. Hili ni tukio la Lushoto mkoani Tanga.

“Oktoba 2024 huko Ruvuma Tanzania familia moja imemzika akiwa hai Baba yao mzazi kisa kwa kumtuhumu kumuua kwa kumroga mwanawe wa kumzaa.”

 

Haya ni ya Tanzania ya hivi sasa, Mwanakwetu bado imani katika ushirikina imekita mizizi.

 

Dkt Simeon Mesaki katika utafiti wake anarejea visa vingi vya masuala ya kustajabisha wakati wa ujamaa ambayo yanalingana na hata visa vya leo hii.

 


Kujishughulisha sana na uchawi kumefanywa kuwa suala la kitaasisi hivi hata mtoa maoni mashuhuri ameinua hali hiyo hadi kufikia kiwango cha ‘utamaduni’ (Okema, Business Times, Agosti 4, 1989).  Baadhi ya Vipindi tofauti vina vilivyorekodiwa kwa namna ya kipekee mno mathalani;Mnamo Aprili 1992, mamlaka za Mkoa wa Kilimanjaro ziliwekwa katika hali mbaya sana zilipolazimika kuamua kumruhusu mganga wa kimila kuendelea na kuwaokoa vijana waliotekwa nyara. na mchawi kama Zombi katika msitu karibu na mji wa Moshi. Kwa mshangao wa watu wengi, Mkuu wa Mkoa wa Mkoa huo wakati huo alimruhusu mganga huyo kufanya kazi yake (kufanya vitu vyake) vya kuwarudisha wahanga hao kwa gharama za serikali.’Haya ni Daily News Aprili 16, 1992 na Uhuru Aprili 16, 1992 haya ni yalikuwa magazeti serikali ya Tanzania wakati huo. Katika kufanya uamuzi huo usio wa kawaida, alisema kuwa serikali ‘ haikuamini uchawi’ na kusema kuwa ingawa ‘haikuondoa ukweli unaowezekana wa jambo hilo na inahitaji ushahidi madhubuti na kupata ripoti ya mwisho juu ya kesi hiyo.’ Mwishowe, hakuna waathiriwa wanaodaiwa kupatikana, wala serikali haikumshtaki mshukiwa wa uchawi, kwa sababu ya kutokuwa na ushahidi wa kutosha. Kweli, mtuhumiwa wa mchawi, Rehema Daudi, alijigamba kwa kuifungulia serikali mashtaka ya kumkashifu. Hapa msomaji wa Mwanakwetu unaweza kurejea gazeti la Mzalendo, Septemba 20, 1992.

 

Kwa upande mwingine, katika kesi isiyo ya kawaida ya mwaka 1991, mahakama ya mwanzo katika manispaa ya Tabora ilitoa uamuzi wa kumlipa fidia mwanamke mmoja wa mjini Tabora aliyedai kuwa tawi la chama tawala.


 

(Chama Cha Mapinduzi-CCM)kilimtuhumu kwa uwongo kuwa anafanya uchawi na kumlazimisha kuhama mjini, haya unaweza kurejea gazeti la Mfanyakazi la Juni 13, 1992. Mwanzoni mwa mwaka 1992, wanavijiji wengi wa wilaya ya Songea walipitisha njia mpya za kutumia haki zao za kidemokrasia kwa kufanya mikutano na kupiga kura ili kubaini nani kati yao ni mchawi. Kutokana na hali hiyo, michango ilitolewa ili kuwawezesha waliotajwa kuwa wachawi kusafiri hadi kwa Bibi Kalembwana, mtaalamu wa masuala ya uchawi huko Mahenge Wilayani Ulanga, kwa ajili ya ibada za ‘kusafisha’

 

Mwezi Aprili mwaka huo huo, vijana thelathini na sita wenye umri kati ya miaka 16 na 30 wa kijiji cha Namabengo, wilayani Songea, walikabiliwa na kesi ya mauaji kwa kumuua Gabriel Malembo (65) ambaye walidai.alihusika na vifo vya vijana wengi kijijini kwao haya yamenukuliwa kutoka gazeti la Uhuru la Aprili 7, 1992. Hatua hizi na zile zinazomhusisha Bi Kalembwana, zilizua taharuki katika duru za serikali za wilaya, si tu kwa sababu ya uvunjifu wa moja kwa moja wa amani bali pia kutokana na athari mbaya za kiuchumi za wateja ambazo Bibi wa Mahenge aliwavutia.

Mnamo Februari 1992 polisi wa Mbeya mjini walilazimika kutuliza ghasia za watu takriban 2,000 waliokuwa wamekusanyika kurusha mawe kwenye nyumba na gari la mtu maarufu mjini hapo. Uvumi kwamba mkazi huyo alikuwa amehifadhi mafuvu ya kichwa na mifupa ya binadamu ambayo inadaiwa alikuwa akiitumia kwa ajili ya uchawi haya yaliripoyowa na gazeti la uhuru la Februari 27, 1992.

 


MAREHEMU ASKOFU MKUU WA  ZAMANI WA MWANZA MHASHAMU  ANTONY MAYALA.


Huko hapa mkoani Mwanza kulikuwa na hekaheka ya kuwaondoa watuhumiwa wa uchawi katika mikoa ya kanda ya ziwa hasa Mwanza na Shinyanga kama ilivyoripotiwa na Daily News Septemba 5, 1990. Kwa hakika haya mambo ni mazito hata katika utafiti wake wa Wazaramo wa Dar-es-Salaam, Lloyd Swantz  mwaka 1990 aligundua kuwa waganga 700 wa dawa za kienyeji waliorodhesha uchawi kuwa wa pili kwa wateja wao. tatizo kubwa zaidi. Kulingana na uchunguzi wake,

 

"...karibu kesi 5,000 kila siku huko Dar-es-Salaam zilihusu shutuma za uchawi na ulozi"

 

Swantz alichukulia takwimu hizi kuwa zenye matatizo sana katika jiji la Dar-es-Salaam. Wasiwasi wake ulirudiwa na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Dar-es-Salaam alipokuwa akiwaonya wakazi wa jiji hilo kwa kuambiwa bahati zao na wapiga ramli, wapiga ramli au wapiga ramli. Badala yake, aliwataka kutumia huduma za bure zinazotolewa na hospitali za serikali haya ni ya Uhuru Mei 23, 1990.

Haya ndiyo mambo ya ushirikina nchini Tanzania ambayo waamini wake ni wengi hata wasomi , wanasiasa, viongozi ,viongozi wa dini huu mchanganyiko maalumu.

 

Mwanakwetu anasema nini siku ya leo?

 

Msomaji wangu huo ndiye ushirikina na mahusiano yake katika shughuli za kiserikali na za kijamii. Kwa Tanzania ya leo suala la ushirikina na mauwaji ya watu yanakwenda sambamba na masuala ya watu wasiojulikana.

Hili ni jambo jipya na geni. Je wanaotekwa, na kuuwawa siyo kwamba mtu anakwenda kupiga chabo sehemu(ramli) akishajua huko na kupata jawabu fulani ni mbaya ndiyo anateka na kumfisha?

Hilo ni swali, swali lengine la kujiuliza je kwanini haya matukio yanatokea sambamba?Je watu wasiojulikana ni kundi jipya la aina ya ushirikina wa kisasa? Kwa hakika Watanzania tunalo jukumu la kujiuliza na kupata majibu.

Kama Baba Mtakatifu Yohane Paulo wa II angekuw a hai mpaka leo alafu angekuja Tanzania kwa hakika angeiambia Tanzania.

“Wapendwa katika Kristo sasa mna aina upya ya Ushirikina ambayo ni watu wasiojulikana.”

 

Mwanakwetu Upo?

Kumbuka- Wasiojulikana Aina Mpya ya Ushirikina.

 

Nasema,

Ahlan Wa Sahlan.

 

makwadeladius@gmail.com

0717649357

 

 


0/Post a Comment/Comments