Adeladius Makwega-MWANZA
Mara zote Mwanakwetu amekuwa akisema kuwa alishuhudia baadhi
ya watumishi wa umma ambao sasa wamestaafu wakati wakitoa maoni yao kwa wabunge
wao juu ya kuundwa kwa Mfuko wa Bima ya Afya (NHIF) ambapo kwa hakika watumihsi
hao wa umma ambao wengine wamefariki na lakini wengine wapo hai huku wamestaafu,
shaka zao ya wakati huu, ambapo Mwanakwetu alikuwa kijana sasa ameamini kuwa mashaka ya
ndugu yale yalikuwa sahihi.
Mwanakwetu anakumbuka kisa hiki,
“Ulikuwa mkutano wa kampeni za CCM baada ya jina lililopitishwa
na CCM la ubunge kwa jimbo la Kasulu kufariki katika ajali ya gari . CCM
waliketi upya na kumchagua marehemu Francis Musati ili wana wa Kasulu wapate kiongozi
wao. Hapo hapo alipitishwa marehemu Francis Musati alifika Makere ambapo ndipo
kijiji alichozaliwa kuanza kampeni. NCCR Mageuzi wakimsimamisha Francis Nzasikwago.
Francis Musati siku hiyo iliyokuwa Jumapili asubuhi kwanza alisali Kanisa
Katoliki la Makere. Hapo Kanisani Mwanakwetu alisali pia na baadaye kufanyika
mkutano mkubwa wa kampeni za CCM stend ya Mabasi ya Makere jirani na msufi
mmoja mkubwa.
Mwalimu Daudi Ruhinda na Mwalimu Rajabu Hussein walihoji juu
ya NHIF kwa marehemu Francis Musati ambaye alikuwa mwanasheria kwa taaluma akasema
, ‘Hilo
nitalifanyia kazi , lakini jukumu lenu ndugu zangu, watu wa Makere ni kunipigia
kura tu.’ Mwisho wa siku Francis Musati alishinda na kuwa mbunge wa
Kasulu.”
Wakati wa kuanzishwa kwa NHIF yalisemwa mengi na walioshika
vipaza sauti walitoa sifa tele sasa wamekaa kimya pengine hawana nafasi hizo
tena, hiyo sasa ni karibu miaka 24. Huu ni umri wa kijana mwenye familia.
“Huu mfuko utakuwa mkombozi wa matibabu ya wafanyakazi.”
Waungaji mkono ambapo walikuwa na
nafasi, wakilinda nafasi zao walisema, huku sasa wajukuu zao sasa wanapata tabu.
Miaka minne baadaye yaani 2004, Mwanakwetu akaingia Utumishi
wa Umma na mwaka 2005 akawa mwanachama wa NHIF bila ya kujaz fomu mshahara wake
wa shilingi 100,800/-ulikatwa pesa za mfuko huo.
Mwaka huu 2023 Bunge la Jamhuri ya Muungano la Tanzania limepitisha
hoja /muswada wa wa Bima ya Afya Kwa wote, hilo mwanakawetu hana shaka nalo. Kinachofanyika
ni kupitisha yatayokuwa yanaaminika yatatoa muelekeo wa matibabu hayo kwa wote.
Mwanakwetu anaamini kuwa jina la Bima ya Afya kwa Wote
lenyewe lina maana na kuwavutia wengi kuwa sasa ni mkombozi wa Watanzania wote
lakini kuna maswali mengi ya kujiuliza,
“Je matumaini hayo kwa watu wote yanaweza kufikiwa kweli na
Watanzania wote wakatibiwa kila ugonjwa walio nao kama ilivyokuwa nyakati za
UJAMAA? Kama matumaini ya Bima ya Afya ya NHIF yakiwa bado yanajikokoja kwa
kundi dogo, vipi kwa kundi kubwa kama hilo?Au tunataka tuanze na jina zuri
alafu baada ya miaka mitano kelele kila kona alafu watu watasema.’ Jamani nchi
hii kubwa, ina watu wengi , suala la afya ni gumu jamani kila mmoja ajitibie
mwenyewe !’ ”
Mwanakwetu leo hii anaamini kuwa ,
“Kwa uzoefu wangu mdogo wa mwaka 1999 na 2000 ninapata picha
ya NHIF kama jembe lisilo na makali , huku sasa dhana ya Bima ya Afya Kwa Wote
naiona kuwa ni Jembe lenye makali ambalo lipo dukani, wakati hata huyu mkulima
hana uwezo wa kulipata, lakini mkulima huyu amejazwa na matumaini kuwa sasa
atapata jembe lenye makali.”
Mwanakwetu anaamini kuwa NHIF hata kama ni jembe lisilo na makali
lakini linaweza kulima hata hatua moja, dhana ya kujenga matumaini makubwa kwa
jembe linalodhaniwa kuwa lina makali ambapo lipo dukani siyo dhana sahihi.
Mwanakwetu anashauri kuwa hili Jembe Lisilo na Makali
libaki likilima hata hiyo hatua moja kidogo kidogo, nalo hilo Jembe
Lenye Makali wakati mipango yake ikikamilika mkulima apewe na lianze
kazi. Mipango ikamilike. Huko kusaini sheria na vikao haina maana yoyote kwa
Mtanzania mgonjwa.
Dhana ya Bima ya Afya Kwa Wote isitumike kuupiga shoka na kuuuwa
mfuko wa NHIF, hilo ni kosa kubwa ambalo pengine baadhi ya wajanja wanaweza
kutumia kuficha madhaifu ya NHIF na madhaifu ya utendaji .
Mwanakwetu anapata picha hii,
“Kumbe NHIF ilikuwa ikifanya uwekezaji mkubwa wa majengo
makubwa makubwa ili kuweka misingi kwa BIMA YA AFYA KWA WOTE? Wanachama wake
wanapata tabu, wanasumbuliwa kumbe kuna kitu mbele yake! Nimetembelea tovuti ya
NHIF sasa imeanza kutumiwa kupachika habari za BIMA YA AFYA KWA WOTE. Hilo ni suala
la Wizara ya Afya na siyo la NHIF“
Mfuko NHIF uendelee , pesa zake , rasilimali zake, mtaji wake
, majengo yake na wanachama wake, watumishi wake waendelee na na mfuko wao huku
BIMA Y AFYA KWA WOTE ianze kazi kwa kila kitu kipya na rasilimali zake mpya.
Isije ikafika mwaka 2050 kwa wale watakao bahati kuwa hai,
mfuko huu wa Bima y Afya Kwa Wote umekufa.
Kikubwa siyo kuundwa kwa taasisi au kubadilisha majina, kikubwa
Watanzania watibiwe bure ili waweze kuendesha maisha yao na waweze kushiriki
vizuri katika shughuli za maendeleo kama ilivyokuwa wakati wa UJAMAA.
Mwanakwetu Upo?
Jembe la Zamani na Jembe Jipya yote yabaki shambani yafanye
kazi na kila jembe na ngwe yake.
Nakutakia Siku Njema.
0717649257
Post a Comment