Lucas Masunzu- Shinyanga.
IMEKUWA kawaida kwa Nduguyetu kuwa shahidi wa kuona nduguze
wakisaliti ukaperana kufunga ndoa takatifu na safari ya maisha ya ndoa kianza.
Kumbukumbu zanduguyetu zilimpeleka hadi kwenye ndoa takatifu ya ndugu Baraka
Masatu iliyofungwakatika kanisa mojawapo la Waadventista wa Sabato, na leo hii
wanapongezwa kwakitimiza miaka mitano kavu ya ndoa yao. Nduguyetu alikumbuka
namna watuwalivyoshiriki katika ibada hiyo ya ndoa takatifu huku akikumbuka
vizuri maneno ya
Mchungaji alivyopigia mstari kuwa
“nanyi waume endeleeni
kuwapenda wake zenukama vile Kristo alivyolipenda
kanisa” siku hiyo hilo halikuwa la bwana harusi pekee bali darasa pia
lilikuwepo kwa waume wote waliohudhuria.
Nduguyetu anakuuma sikio siku ya leo kuwa siku ya harusi ni
siku ya furaha mno kwa Wasabato, watu wengi huhudhuria na walivyowakarimu hata
kama hujaalikwa ukiwezakujialika una uhakika wa kuingia mesini na kushiriki mlo
kikamilifu. Kwa sababu ya uhakika huo nduguyetu amekuwa na mahudhurio mazuri
kila panapotokea tukio la namna hiyo.
Hapo hapo Ben akaanza kuimba wimbo huo kwa mluzi;Furaha i
nyumbani, panapo pendo, Hapana machukizo, panapo pendo, Chakula ni kitamu,
mashamba yasitawi,Maisha ni kamili, panapo pendo.
Baadaye akasema; Wimbo huo “Panapo Pendo” ni wimbo 184 katika
kitabu cha nyimbo za
Kristo, ulitungwa na James McNautghton ambaye ni Mkanada. Ni
wimbo wenye ujumbe wa pekee sana kwa familia zetu. Tafakari za kina alizokuwa
nazo James kuhusu umuhimu wa upendo na amani katikafamilia zilimfanya atunge
wimbo huu unaoimbwa leo hii na maelfu duniani. Kuna familia ambazo hazina amani
kabisa, upendo haupo, baba akiingia watoto wote huchagua kujificha ama hukaa
kimya bila kuongea.
Tena kuna familia ambazo baba na mama ni akina Evander na
Tyson, mpaka watoto wanajuta kuzaliwa kwenye familia hizo kwa sababu upendo
haupo. Tunaimba huu wimbo mara kwa mara ili ujumbe wake ufike kwa wanandoa na
familia zote. Siri kubwa ni kwamba ikiwa upendo utatawala nyumbani watoto
watakuwa na furaha, kuna umuhimu mkubwa mno wa kuwa na upendo na furaha katika
familia zetu kwa sababu familia ni karakana pekee ya kuandaa jamii yenye chuki
au furaha.
Usikubali kuwa mzazi ambaye utapoteza furaha ya familia yako.
Nakutakia siku njema, Kwa heri.
theheroluke23@gmail.com,
0762663595
Post a Comment