Adeladius Makwega-MWANZA
Shajara
ya Mwanakwetu ya Agosti 2023 inasimulia kuwa Mwanakwetu alikuwa njiani akisafiri
kutoka Dodoma kuelekea Mwanza, alipofika stendi ya Nanenane Dodoma alikuwa na
begi moja kubwa ambalo wakati linapakiwa dada utingo na kondakta wa basi
alilopanda alisema,
“Kama
kaka mwenye begi kubwa unashuka Mabuki , hapo ni njiani , haufiki Mwanza Mjini, hivyo
begi lako linatakiwa kukaa upande wa mlango na jirani, kwa hiyo nisubiri
hapo alafu nitaliweka baada ya kuliwekea alama ya mwenye begi.”
Kondakta wa basi hili alikuwa binti mwenye siha
nzuri tu na ana nguvu , wala hakuhitaji msaada wa mtu yoyote kupanga mabegi na
masanduku hayo ya abiria.
Zikiwa zimebakia kama dakika tano, binti huyu akasema,
“Kaka
mwenye begi kubwa , njoo naomba nitajie namba ya kiti yako “
Mwanakwetu akataja 43 na dada huyu akapakia
begi na kuandika namba 43 kwa kirumi XLIII kwenye karatasi nyeupe iliyopachikwa
katika begi hilo, naye Mwanakwetu kuingia ndani ya basi hilo la Dodoma Mwanza.
Wakiwa ndani akatokea abiria mwingine na mizigo
mingi, kondakta akaingia ndani ya basi akasema,
“Yule
kaka mwenye begi, kaka mrefu yupo wapi? Nakuomba kidogo maana nahamisha mzigo
wako, uje uone ninapouweka na nakuomba usikae kiti namba 43, kipo kiti kingine
maalumu kwako wewe, abiria wangu mwenye begi kubwa.”
Mwanakwetu alishuka na kwenda chini ya basi na
begi lake likatolewa na kuwekwa mabegi na masanduku kadhaa, alafu begi la Mwanakwetu
likapelekwa katika chumba cha buti kingine mbele ya mlango wa mbele wa abria
maana basi hili lilikuwa na milango miwili ya kushuka na kupanda abiria.
Begi hilo likaandikwa nambari XLVI naye
Mwanakwetu akaambiwa akakae kiti hicho huko nyuma kabisa ya basi hilo.
Kiti hicho kilikuwa na nambari 45 na 46 ziliandikwa
kwa namba za Kiarabu, Mwanakwetu hapo alimkuta binti mmoja amekaa. Safari
ikawa inaendelea vizuri mno, huyu kondakta wa kike alikuwa akizunguka mara akikagua
tiketi , mara akipokea pesa na mara akitoa vinywaji na vitafunwa kwa abiria
wake.
Kila kondakta huyu wa kike akifika alipokaa
Mwanakwetu neno la uchokozi lilimtoka na kumtania Mwanakwetu , hapo Mwanakwetu
alibaini kuwa binti huyu alikuwa mtundu sana tangu alipokuwa mdogo.
Abiria
mwenye begi kubwa sijakupa pipi yako eeh.
Abiria
mwenye begi kubwa soda yako hii hapa
Abiria
mwenye begi kubwa anakunywa pepsi!
Utani huo wa kondakta huyu ulisababisha abiria
binti kando ya Mwanakwetu ashangae mbona kondakta huyu hana soni na ana nini na
huyu abiria mwenye begi kubwa? Binti huyu akauliza unamfahamu huyu kondakta? Mwanakwetu alijibu hapana.
Utani huo wa kondakta kwa abiria mwenye begi
kubwa na swali la dada abiria kando uliibua maelewano makubwa baina ya
Mwanakwetu na huyu abiria mwenzake. Binti huyu bila hiana alimjibu Mwanakwetu
kila swali alilouliza likiwamo namba ya simu, jina na kazi anayofanya.
“Mimi
ni mwanachuo wa chuo cha Diplomasia Kurasini na nipo njiani kwenda nyumbani kuna
msiba wa mjomba .”
Kumbe unasoma Diplomasia Kurasini !
Je unamfahamu Dkt Jacob Nduye?
(Dkt Nduye)
Mwanakwetu aliuliza.
Binti huyu alijibu kuwa anamfahamu ni mhadhiri
wao, Binti huyu alifurahi mno abiria mwenye begi kubwa kumfahamu Dkt Nduye ,
alafu akamuuliza wewe unamjulia wapi Dkt Nduye? Au alikusomesha.
“Yule
ni kaka yangu kabisa, tunatoka wote kwetu Morogoro sisi ni vitukuu wa Chifu
Morogoro .”
Binti huyu akamuuliza swali lingine, abiria mwenye
begi kubwa jina lake halisi unaitwa nani? Mwanakwetu alijibu kwa kumpwaga
“Mimi
naitwa Melkizadeki Nduye aka Kuhani Mkuu.”
Binti akawa anacheka sana, alafu akauliza
mbona , mbona nyinyi wachangamfu sana ? Hata Dkt Nduye ni mchangamfu sana kama
wewe .
“Sisi
tunazaliwa katika ukoo wa chifu Morogoro, sisi hiyo Morogoro mali yetu, hivyo
ukoo wa machifu mnapokea wageni wengi, kila siku kwa hiyo lazima uwe chakalamu
na siyo mnyonge mnyonge.”
Binti anacheka, mara kondakta anakuja anasema
ahaaa kaka mwenye begi kubwa unanikwepa au umeshapata mwingine?
Mwanakwetu hakusema neno alikaa kimya tu.
Baadaye Mwanakwetu akamwambia ukweli binti huyu
kuwa Dkt Jacob Nduye alifanya naye kazi
TBC Taifa akiwa ni mtangazaji na mtayarishaji mzuri sana wa vipindi vya redio .
Binti akauliza ni kweli alikuwa akitangaza
eeeh? Mwanakwetu akajibu ndiyo na vipindi vyake vilikuwa Mtaalamu na Wetu, Biashara
na Uwezeshaji na hata mada za kuwahoji viongozi na kazi
hiyo aliifanya vizuri sana.
Binti huyu akauliza swali lingine eeeh kwani
alikuwa anapenda nyimbo gani?
“Mimi
nimefika TBC Taifa nilimkuta Seleiman Muhogora , Malima Ndelema, Abisai
Stephern ,Abdul–Rahamin Nzota, Sued Mwihyi hawa ndiyo walikuwa watayarishaji vipindi
na watangazaji wakiume kidogo wakubwa na wale wenye umri wa kati alikuwepo Dominiki
Mrikoni , Benedict Komba , Alex Magwiza na Jacob Nduye.”
Binti akasema naomba nitajie nyimbo alizokuwa
akizipenda kucheza akiwa studio.
“Nduye alipokuwa zamu studioni alizipenda
nyimbo mbili ya kwanza ni Samahani ya Uwongo.”
Nilidhani
kwamba utanisaidia katika matatizo ya dunia,
Kumbe uwongo
Ukiwa
kama rafiki yangu mpenzi wa jufa na kuzikana duniani,
Kumbe
uwongo
Matokeo
yake, huna hata aibu ,unaniomba samahani
Kumbe
uwongo
Binti huyu akawa anaandika jina la wimbo huo
na baadhi ya mashairi yake kwa ufupi katika simu yake ya kiganjani.
(Tancut Almas)
Kumbuka msomaji wangu Mwanakwetu yupo safarini
akitoka Dodoma kwenda Mwanza na anashuka Mabuki.
Binti huyu aliomba atajiwe wimbo mwingine aliyokuwa
akiupenda na kuucheza sana Dkt Jacob Nduye akiwa studio za TBC Taifa.
Ninakwenda
safari, safari yenyewe safari ya kikazi
Najua
hapa utabaki watasema mengi
Pia
wabaya wetu mama watafurahi
Lakini
usisikie ya hao mama watoto
Ninakwenda
kutafuta maisha ya watoto wetu
Chunga
watoto, mama nitarudi, tutaonana kwa mapenzi ya Mungu
Chunga
watoto mama nitarudi , Tutaonana kwa mapenzi ya Mungu
Safari siyo kifo mama yelele
Subiri
nitarudi mama watoto
Nikirudi
mama nitakuletea zawadi, zawadi mama watoto
Nikirudi
mama nipokee kwa mikono miwli,
Huyu mwamafuzni alikuwa anafurahia hasa ujumbe
wa nyimbo hizo ambazo zilizokuwa zinachezwa na Dkt Nduye akiwa mtangazaji
ambapo Mwanakwetu alimshuhudia , hizo zikiwa nyimbo zilizoimbwa na Tancut
Almasi ya Iringa Tanzania , Huku huu wimbo wa mwisho unaitwa Masafa
Marefu.
Msomaji wangu safari inaendelea na Mwanakwetu alibaini kitu,
“Dkt
Jacob Nduye anakaa vizuri na wanachuo hao na kama anafundisha basi anatoa alama
za masomo kwa haki.”
Kama angekuwa ana shida mhadhiri huyu binti
huyu asingevutiwa kabisa na habari za msomi huyu zilizosimuliwa na Mwanakwetu..
Hapo safari iliendelea na Mwanakwetu akapitiwa na
usingizi kwamuda mrefu lakini baadaye akamsikia kondakta akimuamsha huku akimuita
,
“Kaka
mwenye begi kubwa, kaka mwenye begi kubwa basi limefika Mabuki shuka shuka
kaka.”
Mwanakwetu alikurupuka usingizini na kushuka
basini, nalo begi lake kushushwa na kungoja mabasi ya safari ya Malya Kwimba
mkoani Mwanza.
Mwanakwteu Upo ?
Nakutakia siku Njema.
0717649257

Post a Comment